dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, June 13, 2013

Mwani wakosa soko Zanzibar

NA MWINYI SADALLAH

13th June 2013


Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Manzrui
Zao la mwani limeanza kukosa soko visiwani hapa na  kutokana na mahitaji yake kuwa madogo katika soko la Dunia ikilinganishwa na kiwango kikubwa kinachozalishwa na wakulima wa Unguja na Pemba.

Hayo yalisemwa jana na  Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui wakati akijibu swali katika Kikao cha Baraza la Wawakilishi kilichoanza jana  Chukwani kisiwani Unguja.

Mazrui, alisema  wakulima wa mwani wameanza kuathirika na ukosefu wa soko la uhakika na kusababisha kubakia na shehena ya mwani mkavu kwenye nyumba mwao.

Alisema kwamba bahati mbaya Mwani unapokaa muda wa miezi minne tangu kuvunwa bila ya kuuzwa,  kiwango cha ubora upungua.

Alisema  wakati umefika kwa mwani kutumika kama malighafi ya kuzalisha bidhaa nyingine kama vyakula, sabuni badala ya kuuza kama ulivyo katika soko la Dunia.

Akijibu swali la msingi la Mwakilishi wa Viti Maalum, Bikame Yussuf Hamad, Naibu  Waziri wa Wizara hiyo, Thuwaiba Endington Kisasi, alisema  Wizara yake imeanza kufanya utafiti wenye lengo la kusarifu Mwani  nchini kabla ya kuuzwa nje.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment