NA MWANDISHI WETU
21st June 2013
Kamanda wake, Frasier Kashai alisema kuwa watuhumiwa hao (majina tunayo), walikamatwa bunduki tatu aina ya SMG , Shortgun mbili na magobori 29 na risasi 61 Juni 17 mwaka huu saa 12 jioni katika Kijiji cha Lusohoko Wilaya ya Kibondo.
Alisema kukamatwa kwao kunatokana na msako wa polisi baada ya kukithiri kwa matukio ya kuteka magari na unyanganyi wa kutumia silaha katika barabara kuu wilayani humo.
Alisema katika matukio hayo, watu wawili walijeruhiwa kwa risasi kupigwa risasi katika Vijiji vya Kibingo na Biturana na kuporwa mali.
Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Ngendabanyi kwa Andrea (35) kwa kupigwa risasi mguu wake wa kulia na Mathias Christopher (45) mkono wa kushoto kisha kulazwa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo kwa matibabu.
Alisema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment