NA ELIZABETH ZAYA
27th August 2013
Akizungumza wakati akipokea hundi ya fedha hizo, Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa, alisema wamepokea fedha hizo ambazo ni kati ya bilioni 654.7 walizoahidiwa na Jumuiya hiyo mwaka 2009.
Alisema tangu kipindi hicho mpaka sasa, tayari serikali imepokea Sh. bilioni 507.7
Baadhi ya maeneo yaliyopewa kipaumbele katika msaada huo ni sekta ya elimu, afya hususani kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto, maji na sekta ya miundombinu.
“Tunahitaji kuwa na kasi ya kuondoa umaskini, na ndiyo maana tunaamua kuzungumza na wenzetu ambao tunashukuru wametusaidia,” alisema.
Kadhalika, alisema lengo la serikali ni kuweka mikakati ya kupunguza utegemezi wa misaada kutoka nje. Kadhalika alisema deni la serikali linalotokana na mikopo mbalimbali za nje ni Sh. trilioni 41.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment