Afisa Mkaguzi wa Ardhi Zanzibar Shawana Suod Khamis amewataka wananchi kutoa
mashirikiano katika kufanikisha zoezi zima la Utambuzi na usajili wa ardhi nchini.
Kauli hiyo imetolewa jana katika ukumbi wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo wakati akifunga mafunzo ya siku moja ya utambuzi na usajili wa ardhi kwa waandishi wa habari .
Alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuweza kuwapa mbinu za kisasa na uwelewa mpana
kwa waandishi ili kuweza kuihamasisha jamii kuhusiana na zoezi hilo.
Alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Finland kupitia
mradi wa SMOLE II unaendelea na zoezi la usajili wa Ardhi kupitia maeneo mbali mbali ya Zanzibar.
Shawana ameyataja baadhi ya maeneo ambayo tayari yameanza zoezi hilo na kuonyesha
mafanikio kuwa ni Kijiji cha Nugwi , Jendele, Paje, Chwaka, Kwaalinatu ,Mji Mkongwe, Mkokotoni ,Mwembetanga , Rahaleo, Muembeladu, Muembeshauri, Gulion, Kibondeni,
Kisima Majongoo, Mchangani na Vikokotoni .
Akieleza baadhi ya faida za usajili wa ardhi kuwa ni kupunguza migogoro inayotokea mara
kwa mara katika jamii na kumsaidia mmiliki wa ardhi katika kupata mikopo katika benki,
mashirika na taasisi mbali mbali.
Mkufunzi wa mafunzo hayo Afisa Habari na Mawasiliano wa SMOLE Ali Rashid Salim
amesema migogoro mingi ya Ardhi husababisha usheleweshaji wa mirathi kwa jimii hasa
kwa wanawake watoto yatima na watu wenye ulemavu na kupelekea kukosekana kwa
haki kwa wahusika.
Zoezi la usajili wa ardhi limeanza rasmi mwaka 2008 inatarajiwa kuwa ifikapo mwaka
2015 asilimia 50 ya ardhi yote ya Zanzibar iwe tayari imeshasajiliwa .
Idara ya habari maelezo
Chanzo: ZanzibariYetu
No comments :
Post a Comment