zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, September 30, 2013

Rais Dk. Shein aipongeza China miaka 64 ya uhuru

NA MWANDISHI WETU

30th September 2013


Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein
Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping, kwa kuadhimisha miaka 64 ya uhuru wa nchi hiyo.

Katika salamu zake hizo, Rais Dk. Shein, amesema wananchi wa Zanzibar wanaungana na ndugu zao wa China katika kusherehekea miaka 64 ya uhuru wa nchi hiyo pamoja na urafiki na mshikamano uliodumu kwa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili.

Aidha, ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa mafanikio makubwa iliyoyapata katika sekta zote za maendeleo chini ya uongozi imara wa Chama cha Kikomunisti cha nchi hiyo.

Alielezea matumaini yake kuwa ushirikiano baina ya Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na wananchi wa Zanzibar utaendelea kuimarika zaidi.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment