Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuashiria kuweka
Jiwe la Msingi katika benki ya Maendeleo PLC, wakati wa hafla ya
uzinduzi rasmi wa benki hiyo, iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Kulia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dkt. Alex Malasusa (kushoto)
ni Naibu Waziri wa Fedha,Janeth Mbene
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuashiria kufungua
benki ya Maendeleo PLC, wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa
benki hiyo, iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Askofu
Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dkt. Alex Malasusa (kushoto) ni
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadic na Naibu
Waziri wa Fedha,Janeth Mbene.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa ufunguzi
rasmi wa bemki hiyo,leo
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla
hiyo ya ufunguzi wa benki hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, Afisa Utawala
wa Benki ya Maendeleo, Rose Mushi, ambaye ni mmoja kati ya
waanzilishi wa benki hiyo na wahamasishaji kwa watu
kununua shea katika benki hiyo, ambapo walifanikiwa kupata
jumla ya Sh. Bilioni 4.5. Makamu alikabidhi vyeti hivyo wakati wa
hafla ya uzinduzi rasmi wa benki hiyo iliyopo jijini Dar es Salaa,
leo Nov 12, 2013. Wa pili (kushoto) ni Naibu Waziri wa Fedha,
Janeth Mbene (kulia) ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT,
Dkt. Alex Malasusa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, Mchungaji,
George Fupe, ambaye ni mmoja kati ya waanzilishi wa benki
hiyo na wahamasishaji kwa watu kununua shea katika benki hiyo,
ambapo walifanikiwa kupata jumla ya Sh. Bilioni 4.5. Makamu alikabidhi
vyeti hivyo wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa benki hiyo iliyopo jijini
Dar es Salaa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi mfano wa kadi ya ATM,
mteja wa kwanza kufungua Account katika benki hiyo,
Elianasa Marco Njiu,mkazi wa jijini Dar es Salaam,
wakati wa hafla ya ufunguzi wa Benki hiyo iliyofanyika jijini
Dar es Salaam, leo Nov 12, 2013. Wa pili (kulia) ni Mteja wa
kwanza kupata mkopo katika benki hiyo, Margareth Chiwata
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na
baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo na wachungaji wa
Kanisa la KKKT, baada ya ufunguzi rasmi wa benki hiyo.
Picha na OMR
Chanzo: ZanziNews









No comments :
Post a Comment