NA JUMA NG'OKO
4th December 2013
Kikwete alitoa rai hiyo juzi wakati akizindua Tawi la Benki ya Azania Limited katika Kijiji cha Lamadi kilichopo Wilaya ya Busega mkoani Simiyu mapema wiki hii.
" Fedha haziokotwi barabarani, na wala huwezi ukanyeshewa na fedha kama mvua.
Fedha za uhakika kwa ajili ya biashara endelevu hutokana na mikopo katika taasisi za kifedha," alisema Kikwete huku akiwaasa wananchi wasiogope kukopa ili mradi wazingatie kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.
Alisema fedha ni kichocheo muhimu sana cha maendeleo ya kila binadamu na kwamba Serikali yake itaendelea kushirikiana na taasisi za fedha, ikiwamo benki hiyo kuhakikisha uchumi wa mtu mmoja mmoja, kaya hadi taifa unakuwa kwa kasi kadri inavyowezekana
Aliwataka wakazi wa kijiji hicho na vya jirani kufungua akaunti katika benki hiyo na kuomba mikopo itakayowasaidia kuanzisha miradi ya biashara na kuwa na maisha bora.
" Ninawapongeza sana Azania Benki kwa kutambua umuhimu wa kuwekeza huduma za kibenki, hasa maeneo ya vijijini, " alisema na kuongeza kuwa hatua hiyo itawavutia wawekezaji wengi zaidi katika maeneo ya vijijini na kasi ya wananchi kujiletea maendeleo.
Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Charles Singili, alisema ufunguzi wa tawi hilo katika kijiji hicho ni sehemu ya kutekeleza agizo lililotolewa na Rais Kikwete wakati akifungua tawi lao Mwaloni-Kirumba jijini Mwanza mwaka 2006.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment