zanglassworks

zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, November 2, 2014

FUJO NA NGUMI KWENYE MDAHALO WA KATIBA!



Jaji Warioba.

NGUMI ZAPIGWA WAKATI WA MDAHALO WA KATIBA

VURUGU zilizoambatana na ngumi kurushwa zimetokea hivi punde katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alipokuwa akitoa mada kwenye mdahalo wa kujadili umuhimu wa kuielewa kwa kina Katiba inayopendekezwa kama ilivyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba.

Vurugu hizo zimezuka baada ya watu waliokuwa na mabango kuvamia ukumbuni hapo na kusababisha baadhi ya watu waliokuwa wanafuatilia mdahalo huo kuwakabili na kuwapa kichapo.

Baada ya vurugu hizo, mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kurushwa moja kwa moja na ITV umesimamishwa kwa muda. 


Habari kwa hisani ya GPL
Chanzo: Vijimambo:

Picha zote zifuatazo ni kwa hisani ya blog la Kajunason

VIJANA WAVAMIA MDAHALO WA KUJADILI KATIBA INAYOPENDEZWA, WATAKA KUMPIGA MZEE WARIOBA


Jaji Joseph Warioba akitoa mada.


Mtoa mada katika mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa, Jaji Joseph Warioba akitoa mada kabla ya mkutano huo kuvunjika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Saam leo. (Picha zote na Francis Dande).

Baadhi ya vijana walioingia na mabango ndani ya ukumbi wa mkutano
wakiwa na mabango yaliyokuwa yakisomeka ‘Katiba inayopendekezwa tumeipokea tunaiunga mkono’.

Mlinzi wa Jaji Joseph Warioba (kushoto) akimkinga kwa mikono ili asipate
madhara baada ya mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa kuvamiwa na kundi la vijana na kusababisha uvunjifu wa amani. 

Jaji Joseph Warioba akiangalia usalama wake kabla ya kuondolewa mlinzi
wake katika ukumbi wa Ubungo Plaza ambapo mdahalo wa kuijadili Katiba
inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika kabla ya kuvunjika.

Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akimzuia mmoja wa vijana aliyekuwa na jazba mara baada ya kutokea kwa vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekeza.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku (katikati) akisindikizwa kuingia katika chumba cha VIP mara baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa. Mdahalo huo uliandalia na taasisi hiyo.

 Vijana wakiwa na mabango.


 Mabango yakiwa juu.


 Vujo zinaanza.


 Mmoja wa vijana waliokuwa wakitoa maneno ya kashfa kwa Jaji Warioba akiwanyooshea vidole viongozi wa meza Kuu.


 Baadhi ya viti vilivyovujwa.


 Jaji Warioba akitoka katika ukumbi huku akisindikizwa na askari kanzu.


 Jaji Warioba akisindikizwa na makachero wa Polisi.


 Jaji Warioba akiwapungia mkono wananchi waliokuwa wamefurika nje ya jengo la Ubungo Plaza ambako mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika.

Wananchi walikuwa nje ya jengo la Ubungo Plaza wakimshangilia Jaji Warioba wakati akitoka katika ukumbi wa mdahalo huku wakimuita 'Rais Rais'.


No comments :

Post a Comment