dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, September 8, 2015

Magufuli: Nitaboresha maslahi ya manesi na madaktari

  •  Akiwahutubia wakazi wa Turiani mkoani Morogoro leo, amesema katika Serikali yake atahakikisha anadhibiti ukosefu wa dawa katika vituo vya afya na hospitali ili  kuhakikisha wananchi hawaendelei tena kuandikiwa vyeti na kwenda kununua katika maduka ya dawa.
Tanga. Mgombea wa urais kupitia CCM Dk John Magufuli amesema iwapo atapatiwa ridhaa ya kuingia Ikulu atahakikisha anaboresha maslahi ya manesi na madaktari na kuongeza kuwa hatawavumilia watumishi wote wanaofungia dawa kwenye mabohari mpaka zinaharibika.
Akiwahutubia wakazi wa Turiani mkoani Morogoro leo, amesema katika Serikali yake atahakikisha anadhibiti ukosefu wa dawa katika vituo vya afya na hospitali ili  kuhakikisha wananchi hawaendelei tena kuandikiwa vyeti na kwenda kununua katika maduka ya dawa.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk Magufuli kugusia moja kwa moja mipango yake ya kudhibiti uharibifu wa dawa ambao huripotiwa kufanyika katika Bohari ya Dawa (MSD) yenye dhamana ya usambazaji dawa nchini.
"Tutaboresha masilahi ya manesi pamoja na madaktari ili waipende kazi na kuifanya kwa moyo, wale wanaotoka na madawa kule Dar es Salaam saa  nyingine yanakaa mpaka yanaharibika bila kupelekwa yanakotakiwa. Hao mniachie nitalala nao mbele," alisema Dk Magufuli na kushangiliwa.
Ahadi hiyo hivi leo imeonekana kuwa kete ya ziada ya uboreshaji wa huduma za Afya nchini ambapo aliirudia tena katika mkutano wa Songe wilayani Kilindi.
"Lazima dawa zipatikane hospitali na huyo anayeleta dawa anakaa Dar es Salaam akae 'standby' (akae chonjo) kweli kweli, "  alisema.
Mbali na kuhakikisha dawa zinapatikana wakati wote, mgombea huyo amesema Serikali itapeleka vitanda vya kutosha na kuhakikisha  kila kijiji kina kituo cha afya na kila wilaya ina hospitali.
"Mimi siyo Shehe, siyo padri lakini nchi hii naifahamu vizuri tusibaguane hata kidogo. Tukibaguana, tutaanza dini kwa dini, kabila kwa kabila hata Wapare hapa wakaanza kuondolewa, hatutafika, " alisisitiza Dk Magufuli.

No comments :

Post a Comment