Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 11, 2015

KAKAKUONA: JK umeondoka bila kuumaliza mpasuko Zanzibar?

Image result for KIKWETE

Rais
Jakaya Kikwete alipoingia madarakani 2005, aliahidi kushughulikia mpasuko wa kisiasa Zanzibar, lakini bahati mbaya anaondoka madarakani akiacha mpasuko mkubwa zaidi wa kisiasa.

Kabla sijarejea hotuba yake aliyoitoa Bungeni, 2005, uchaguzi kwa upande wa Zanzibar umeingia dosari baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, kutangaza kuufuta.

Jecha anadaiwa kufanya uamuzi huo bila kuwapo kikao na makamishina wa ZEC kama sheria inavyotaka, lakini uamuzi huu ukionekana kusukumwa zaidi na shinikizo kutoka nje ya tume hiyo.

Mpaka anatangaza kufuta uchaguzi huo kwa sababu alizodai zimeufanya usiwe huru na wa haki, yalibaki kutangazwa  matokeo ya majimbo 14.

Uamuzi huo umepingwa si tu na mgombea urais wa CUF, Maalim Seif Sharrif  Hamad bali hata waangalizi wa kimataifa na Jumuiya za Kimataifa.

Kama ilivyokuwa mwaka 2000, hali ya kisiasa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2005 ilikuwa mbaya  kwa sababu ya matumizi ya vyombo vya Dola kuhakikisha CCM inabaki madarakani.

CUF wakati huo, chini ya mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba ilitoa tamko la kutotambua matokeo yaliyotangazwa na ZEC na kutaka uchaguzi huo urudiwe kwa uangalizi wa Umoja wa Mataifa (UN).

Leo hii watawala wa Zanzibar akiwamo Rais aliyemaliza muda wake kikatiba, Dk Ali Mohamed Shein hawasikii la mtu, wana hamu na madaraka basi.Desemba 30, 2005 wakati Rais Kikwete anaingia madarakani alisema anasononeshwa kwamba anachukua nchi wakati kukiwa na mpasuko mkubwa wa kisiasa visiwani Zanzibar na akaahidi kuutafutia ufumbuzi.
“Nachukua uongozi wa taifa nikiwa nasononeshwa na mpasuko wa kisiasa kati ya Unguja na Pemba na pengine kati ya Pemba na sehemu nyingine za Jamhuri yetu,” alisema na kuongeza;
“Wakati umefika wa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa mpasuko huo. Nategemea kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa wanasiasa wa pande zote wa Zanzibar. Naomba mnielewe dhamira yangu.”
“Nakusudia kufanya kila lililo ndani ya uwezo wangu ili siku awamu yangu ya uongozi wa Jamhuri yetu ikifika ukingoni nisiiache hali hii ya mpasuko wa kisiasa kama nilivyoikuta.”
Ni kutokana na dhamira hiyo njema ya Rais Kikwete, tulishuhudia vyama vya CUF na CCM vikiunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).
Katika hotuba yake ya kulivunja Bunge aliyoitoa Julai 9, 2015,  Rais Kikwete alisema kuundwa kwa SUK kulifanya mpasuko wa kisiasa uliodumu tangu uchaguzi wa mwaka 1995 kupatiwa tiba.
Leo Rais Kikwete akiwa katika siku za mwisho za utawala wake, anataka kuondoka akiiacha Zanzibar katika mtafaruku mkubwa wa kisiasa baada ya watawala kugoma kumtangaza mshindi!
Bahati mbaya, watawala wetu wameweka sheria mbaya ambazo haziruhusu mtu yeyote kuhoji ushindi wa mgombea urais kama ametangazwa na Tume ya Uchaguzi.
Ibara ya 41(7) ya Katiba ya 1977 inasema” Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Rais, hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake”.
Kifungu cha 34 (7) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, nacho kimeweka kifungu kama hicho cha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinachozuia kuchunguza kuchaguliwa kwa Rais.
Sheria hizi ni mbaya kwa kuwa kama kutatokea mgogoro wa kisiasa, hakuna njia ya kuweza kutokea. Tumejenga nyumba tukaweka mageti na kuziba kila mahali.

No comments :

Post a Comment