Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, November 4, 2015

Polisi, Ukawa jino kwa jino

Polisi wakiwa kwenye doria jijini Dar es salaam
Jeshi la Polisi nchini, limeendelea kupiga marufuku maandamano  yaliyokuwa yamepangwa kuanza kufanywa jana bila kikomo na wafuasi wa  vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupinga  unyonywaji wa demokrasia dhidi ya aliyekuwa mgombea wao wa urais  wake, Edward Lowassa, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema).
Lowassa alishindwa katika uchaguzi huo kwa kupata kura asilimia 39.97  dhidi ya asilimia 58.9 za mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.  John Magufuli, aliyeibuka na ushindi katika uchaguzi uliofanyika  Oktoba 25, mwaka huu Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Makao Makuu  ya Jeshi la Polisi nchini, Paul Chagonja, akizungumza kwa niaba ya  Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, (IGP) Ernest Mangu, aliwaeleza  waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa maandamano hayo  yalikuwa ni batili kwa sababu wafuasi wa vyama hivyo vya Chadema,  CUF, NCCR-Mageuzi na NLD walikiuka taratibu za uombaji wa kibali kwa  kutuma barua ya maombi muda mfupi kabla ya maandamano.
Chagonja alisema kwa mujibu wa taratibu za uombaji wa kibali, unatakiwa kuomba siku mbili au saa 48 kabla ya maandamano.
“Kwanza tulibaini maandamano hayo yanaweza kuwasumbua wakazi wa Jiji  wakashindwa kuendelea na shughuli zao, lakini pia walichelewa  kutupatia barua za kuomba kibali licha ya kuwa zilikuwa zinasema  waliomba Oktoba 31 na Jeshi la Polisi liliwanyima kibali,” alisema  Kamishna Chagonja.
Juzi, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna  Suleiman Kova, alipiga marufu maandamano hayo kwa madai kuwu barua  hiyo haikubainisha muda wa kuanza na mahali watakapopita. Kamishna  Kova alisema: “Kufanya maandamano yasiyo na kikomo haiwezekani kwani  yataathiri shughuli za jijini hapa na kuwapa usumbufu mkubwa wananchi  wa kushindwa kufanya shughuli zao. Vile vile, yanaweza kuleta  uvunjifu wa amani, haiwezekani Polisi wakawa na kazi ya kulinda  waandamanaji tu.” 
KUMWAPISHA MAGUFULI
Sambamba na hilo, Kamishna Chagonja alisema jeshi hilo limejipanga  kikamilifu kulinda usalama wa raia na mali zao katika tukio la  kuapishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dk. John  Magufuli, kesho. 
 Dk. Magufuli alitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuwa  mshindi wa urais Oktoba 29, mwaka huu na kukabidhiwa cheti cha  ushindi Oktoba 30. 
“Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na  usalama,  limejipanga vyema kuhakikisha usalama wa raia na mali zake  unaimarishwa katika siku ya kuapishwa kwa Dk. Magufuli. Tunawaomba  wananchi watupe ushirikiano kwa kutoa taarifa waonapo tukio la  uvunjifu wa sheria,” alisema Kamishna Chagonja. 
Mbali na hilo, Kamishna Chagonja aliwashukuru wananchi kwa kuwa  watulivu katika kipindi chote cha uchaguzi na kuwataka kufanya hivyo  hadi siku ya kuapishwa kwa Rais mpya. 
Pia, alivishukuru vyombo vya habari kwa kutoa ushirikiano na  kuhabarisha umma kwa weledi na kuimarisha amani ya nchi. 
Kuhusu watu waliokamatwa wakati wa uchaguzi kwa makosa mbalimbali,  Chagonja alisema jeshi hilo linaendelea kuwashikilia watu kadhaa,  ambao  hata hivyo, hakutaja idadi yao. 
Alisema wengine wameshapelekwa mahakamani na wakapewa dhamana na  wengine wanaendelea kukamatwa na kwamba hakuna takwimu sahihi za  wanaoshikiliwa. 
KAULI YA UKAWA
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitendo cha Mawasiliano wa Chadema, Tumaini  Makene, alisema barua za kuomba kibali cha kufanya maandamano  ziliandikwa na uongozi wa kanda.
Alisema kwa sasa chama hicho kina jumla ya Kanda 10 hivyo kila kanda  inaweza kuratibu shuguli zake. “Kuhusu masuala ya maandamano unapaswa  kuzungumza na viongozi wa kanda ambao ndio walioandika barua, pia  wanaweza kukueleza kama wameandamana ama la,” alisema Makene.
Nipashe ilimtafuta kwa njia ya simu Ofisa wa Kanda ya Pwani, ambayo  ndio iliandika barua ya kuomba kibali kwenda kwa Jeshi la Polisi,  bila ya mafaniko kutokana na simu yake yake kuita bila ya majibu.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment