zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, March 16, 2017

Rais Uhuru Kenyatta kupunguza mishahara ya wabunge!

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, ametoa wito wa kupunguzwa kwa mishahara ya wabunge na maafisa wakuu akisema viwango vya juu vya mishahara vimesababisha migomo ya wafanyakazi wa sekta nyingine kutaka nyongeza za mishahara.

Rais Kenyatta ameyasema hayo alipohutubia kwenye kikao cha pamoja cha Bunge la Taifa na Baraza la Senate katika hotuba yake ya mwisho ya kipindi chake cha kwanza uongozini.

Hotuba ya Rais huyo imesheheni majibu ya maswali yanayoulizwa na upinzani kila siku kuanzia ufisadi, ufujaji wa fedha za umma, kuzorota kwa huduma za afya, elimu na usalama.
Rais Uhuru amejivunia kupungua kwa visa vya mashambulizi ya kigaidi nchini, kuongezwa kwa idadi ya maafisa wa usalama na ukuaji wa uchumi ambao amesema umekuwa juu ya kiwango cha makadirio ya taasisi za kimataifa cha 3% kwa Mwaka.

Huku zikiwa zimesalia siku 145 kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika Rais Kenyatta ametumia fursa ya hotuba hiyo kujipigia upatu ili aweze kuchaguliwa tena kwa kipindi cha pili.

Rais Kenyatta amesema kwamba serikali yake imejitolea kuhakikisha uchaguzi huru na haki na kuiomba Idara ya Mahakama kutotatiza matayarisho ya uchaguzi ujao.

No comments :

Post a Comment