dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, July 16, 2017

SIKU YA TANZANIA KATIKA JIJI LA OTTAWA, CANADA - 14TH JULY, 2017!

Tarehe 14 Julai, 2017 ilikuwa ni siku ya Tanzania Jijini Ottawa, Canada. Siku hii ilikuwa ni mwendelezo wa sherehe za kuazimisha miaka 150 ya uwepo wa Taifa la Canada. Mamlaka ya Jiji la Ottawa ilitoa fursa kwa ofisi mbalimbali za kibalozi kushiriki katika sherehe hizo ambazo zimekuwa zikiendelea tangu Januari 2017. Tarehe 14 Julai ilipangwa kwa ajili ya Tanzania. Ubalozi wa Tanzania uliopo Jijini Ottawa ulitumia siku hiyo kuitangaza nchi yetu katika nyanja mbalimbali kama vile uchumi, utalii na utamaduni.
Balozi wa Tanzania nchini Canada Mhe. Jack Zoka akijiandaa kukata utepe ili kuzindua siku ya Tanzania Jijini Ottawa, Canada. Kulia ni mke wa Balozi Bi. Esther Zoka na kushoto ni afisa wa Ubalozi Bi. Aisha Mandia akiwa ameshika "tray" iliyokuwa na mkasi.
Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Canada, Jack Zoka akiwa na mke wake Bi. Esther Zoka, akikata utepe kuashiria kuanzishwa kwa shughuli mbalimbali zilizofanyika siku hiyo.
Mhe. Balozi Jack Zoka akiwa na Meya wa Jiji la Ottawa Bw. Jim Watson na Bi. Esther Zoka
Bi. Petronilla Lyimo, Mshereheshaji wa siku hiyo ambaye ni mke wa Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Jumuiya ya Wana-diaspora wa Tanzania Jijini Ottawa (TAO)
Mhe. Balozi Jack Zoka akimtembeza Meya Jim Watson kwenye maonyesho ya vikundi mbalimbali vilivyoshiriki siku hiyo.
Afisa wa Ubalozi Bw. Leonce Bilauli akitoa zawadi kwa Meya wa Jiji la Ottawa Jim Watson alipotembelea ukumbi wa maonyesho akishuhudiwa na Balozi wa Tanzania nchini Canada Mhe. Jack Zoka.
Wakiwa katika picha ya pamoja, Meya Jim Watson akiwa na Mhe. Balozi na Afisa wa Ubalozi Bi. Fortunata Ngoli. Kushoto ni Mke wa Balozi Bi. Esther Zoka.
 Afisa wa Balozi Bi. Aziza Bukuku akiwa kwenye banda la Ubalozi akielezea wageni kuhusu Tanzania 
 Mhe. Balozi Jack Zoka na Bi Esther Zoka wakiwa na mgeni rasmi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Canada Bw. Mark Mostovak wakati wa hafla iliyofanyika jioni.
Balozi wa Tanzania nchini Canada akitoa hotuba wakati wa hafla iliyofanyika jioni
Mgeni rasmi Bw. Mark Mostovac akitoa hotuba kwa niaba ya serikali ya Canada wakati wa halfa ya jioni
Bendi ya "Hapa Kazi tu" wakishangamsha wageni mbalimbali waliofika kujionea na kusikiliza kuhusu Tanzania

No comments :

Post a Comment