dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, December 1, 2017

Wachaga kuanza kuchunguzwa na TAKUKURU!

Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani Hai mkoani Kilimanjaro (Takukuru), imeanza kuchunguza utamaduni wa familia za kabila la Wachaga za kutumia majani kufunika au kumaliza kienyeji kesi zinazohusu ukatili wa kijinsia na mimba za wanafunzi.

Majani hayo maarufu kwa jina la Sale/Masale kwa mila na tamaduni za kabila la Wachaga, hutumika kuashiria amani, kuomba msamaha na kumaliza tofauti zao na mara nyingi hutumika pale kunapokuwa na matatizo baina ya pande mbili.Ofisa wa Takukuru Wilaya ya humo, Denis Mazigo amefichua siri hiyo ya kuanza kwa uchunguzi dhidi ya mila hiyo wakati wa uwasilishaji ripoti ya Kamati ya Ulinzi wa Mtoto.

“Haliwezi kutangulizwa jani la sale peke yake, lazima kuna mazingira ya kutolewa kwa fedha kama rushwa, ndiyo msamaha uweze kukubalika.

"Sasa sisi kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa tumeanza kufanyia kazi jambo hili, kwa sababu tumeona kesi nyingi za ukatili zikikwama huku zikiwa na ushahidi wa kutosha.” amesema Mazigo.

No comments :

Post a Comment