dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, January 5, 2019

Mtanzania apata Tuzo China, aweka rekodi ya kipekee Afrika!



Mtanzania Victoria Mwanziva, amepata tuzo maalumu na utambuzi maalumu kama Mwanafunzi bora katika chuo kikuu cha Harbin Institute of Technology, Mjini Harbin, China ambapo anasoma Shahada ya uzamili yaani Masters in Public Administration.

Victoria Mwanziva amepata tuzo hii ya heshima  akiwa mmoja wa wanafunzi 10 pekee wa Kimataifa waliopewa Heshima Hiyo jimboni hapo na akiwa ni Mwanamke pekee wa kiafrika kuipata tuzo hii.

Mgeni rasmi na aliyekabidhi tuzo hizo ni Mh.Rais wa Chuo cha Harbin , Bw. Zhou (Chancellor Mkuu wa Kampasi zote za HIT China)- aliambatana na viongozi waandamizi wa Chuo hicho na viongozi wa Serikali ya China.

Mwanziva amepata tuzo hii kutokana na mchango wake maswala mtambuka chuoni; kujituma kwake Kimasomo; kupata ufaulu wa juu (Daraja la kwanza).

Victoria Mwanziva anamalizia masomo yake China na kwa sasa anahudumu kama Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Watanzania Nchini China, nafasi hii imempelekea kuimarisha mtandao wa Watanzania wanaosoma China kupitia jumuiya zao za miji wanayosoma.

No comments :

Post a Comment