Hili blog ni kuhusu Tanzania na dunia nzima kwa ujumla.
Pita kila siku kwa habari moto moto.
(This blog is about Tanzania and the world as a whole.
Pass-by everyday for breaking news).
***********************KARIBUNI NYOTE / YOU ARE ALL WELCOME!***********************
Kwarara Msikitini
Dual Citizenship #2
Pemba Paradise
Zanzibar Diaspora
ZanzibarNiKwetuStoreBanner
Mwanakwerekwe shops ad
ZNK Patreon
Scrolling news
Saturday, March 23, 2019
UNICEF yaonya muda unakwisha kwa wahanga wa kimbunga Msumbiji!
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa mataifa la kuwahudumia watoto UNICEF Henrietta Fore ameonya jana kwamba juhudi za kiutu zinazidi kuchelewa kwa mamia kwa maelfu ya watu wa Msumbiji waliathirika na kimbunga Idai kilichopiga wiki iliyopita.
Fore amesema muda unakwisha , na imefikia katika wakati mgumu. Amesema hayo muda mfupi baada ya kuwasili katika mji wa bandari ulioharibiwa na kimbunga hicho wa Beira kutoka New York kutathmini hali katika mji huo.
Umoja wa mataifa umeanzisha miito ya kuomba msaada wakati ukisubiri taarifa za kutosha kuweza kutoa makadirio sahihi ya mahitaji wakati operesheni za uokozi zikiendelea.
Amesema kwamba hatua inayofuata ni kupata maji safi ya kunywa kwa sababu magonjwa ndio kitu kitakachofuatia kwa sababu kuna maji yaliyotuwama, miili iliyoharibika na kuoza, ukosefu wa vyoo na vifaa vya usafi wa mwilini.
No comments :
Post a Comment