Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, March 5, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE AWATAKA WATU WANAOISEMA VIBAYA TANZANIA KUKAA KIMYA SASA!

PROF. KABUDI AANZA KAZI KWA VITISHO!


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, amewataka watu wanaoisema vibaya Tanzania kukaa kimya kwa sasa.

Profesa Kabudi amesema hayo leo Jumatatu Februari 4, Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kuapishwa kuwa waziri wa wizara hiyo na Rais John Magufuli aliyemteua juzi baada ya kufanya mabadiliko madogo ya mawaziri.

“Jana haikuwa siku nzuri kwangu niliamshwa na watu wengine kuambiwa kwamba nimeteliuwa katika nafasi hii, lakini nashukuru kwa kunipa nafasi.
“Huu si wakati wa kuisema nchi yetu, kuibeza na kuipagaza… nchi yetu ilijengwa na mwasisi Mwalimu Julius Nyerere, yeyote Mtanzania mwenye tatizo na nchi hii atutendee jambo moja tu, akae kimya.

“Tuna jambo moja tu kubwa la kujenga mahusiano na wale wanaoitakia mema nchi yetu,” amesema Profesa Kabudi.

Pamoja na Profesa Kabudi, pia Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Augustine Mahiga aliapishwa na baadhi ya Makamishna wa Jeshi la Polisi.
Usikubali kupitwa na habari..Pakua App ya Malunde1 blog HAPA Ili tuwe tunakutumia habari moja kwa moja Kwenye Simu yako

No comments :

Post a Comment