Wadau wa sekta mbalimbali wamekutana kujadili sheria, kanuni zilizopo ili kuboresha usalama wa mionzi hususan katika uchimbaji wa madini ya uranium ili kuhakikisha usalama wa watanzania kiwa ni pamoja na kuwawezesha watanzania kunufaika na madini hayo.
Mkurugenzi wa Tume ya Nguvu za Atomic Tanzani ,Profesa Lazaro Busagala amesema kuwa taasisi mbalimbali zimekutana ikiwemo Tume ya madini,Mwanasheria Mkuu wa serikali na Nemc lengo ni kuwa na sheria na kanuni inayomlinda Mtanzania na kuhakikisha madini yanayanufaisha Watanzania.
Mkaguzi Mkuu wa Migodi na Mazingira kutoka Tume ya Madini ,Abdulrahman Mwanga amesema kuwa madini ya Uranium ni madini yanayoweza kutumika kama chanzo cha nushati pia kutumika kutengeneza silaha kali hivyo uwekaji wa kanuni na sheria utasaidia kudhibiti madini hayo ili yasilete madhara kwa watu na mazingira.
Kamishna Msaidizi wa madini nchini,Terence Ngole amesema kuwa uchimbaji wa madini hayo bado haujaanza nchini kwani ulisimama kutokana na kushuka kwa bei ya madini hayo katika soko la dunia ,kwa sasa wako kwenye mpango wa kuweka kisheria ,kinanuni ili uchimbaji ukianza madhara yasijitokeze.
Mkurugenzi wa Tume ya Nguvu za Atomic Tanzani ,Profesa Lazaro Busagala amesema kuwa taasisi mbalimbali zimekutana ikiwemo Tume ya madini,Mwanasheria Mkuu wa serikali na Nemc lengo ni kuwa na sheria na kanuni inayomlinda Mtanzania na kuhakikisha madini yanayanufaisha Watanzania.
Mkaguzi Mkuu wa Migodi na Mazingira kutoka Tume ya Madini ,Abdulrahman Mwanga amesema kuwa madini ya Uranium ni madini yanayoweza kutumika kama chanzo cha nushati pia kutumika kutengeneza silaha kali hivyo uwekaji wa kanuni na sheria utasaidia kudhibiti madini hayo ili yasilete madhara kwa watu na mazingira.
Kamishna Msaidizi wa madini nchini,Terence Ngole amesema kuwa uchimbaji wa madini hayo bado haujaanza nchini kwani ulisimama kutokana na kushuka kwa bei ya madini hayo katika soko la dunia ,kwa sasa wako kwenye mpango wa kuweka kisheria ,kinanuni ili uchimbaji ukianza madhara yasijitokeze.

No comments :
Post a Comment