dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, January 6, 2020

Al Shabab wanne wauwawa katika shambulizi la uwanja wa ndege Kenya!

Kundi la kigaidi la Al Shabaab limefanya shambulio katika uwanja wa ndege wa jeshi unaotumiwa na majeshi ya Marekani na Kenya eneo la Lamu, kusini mashariki mwa Kenya.

Kundi hilo la kigaidi la mtandao wa Al-Qaeda limesema kuwa tukio hilo halina uhusiano wowote na malumbano yanayoendelea kati ya Iran na Marekani.

Jeshi la Kenya limethibitisha kutokea kwa shambulio hilo katika uwanja wa ndege wa Lamu.

Msemaji wa jeshi la Kenya amesema kuwa wameweza kudhibiti shambulio hilo na wamekuta miili minne ya wanamgambo wa Al Shabaab.

Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.

Al Shabaab walikuwa wanajaribu kuelekea kambi ya karibu inayotumiwa na Marekani na jeshi la Kenya.

Wakazi wa eneo hilo wameripoti kuwa walikuwa wanasikia milipuko na baadae milio ya risasi.

Moshi mzito ulionekana katika eneo la tukio.

Uwanja wa ndege wa Lamu umefungwa kwa muda usiojulikana.


No comments :

Post a Comment