Hili blog ni kuhusu Tanzania na dunia nzima kwa ujumla. Pita kila siku kwa habari moto moto. (This blog is about Tanzania and the world as a whole. Pass-by everyday for breaking news). ***********************KARIBUNI NYOTE / YOU ARE ALL WELCOME!***********************
Saturday, June 6, 2020
NOW ZANZIBAR WELCOMES BACK TOURISTS!
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema kuanzia leo safari za ndege za kitalii kuwasili nchini baada ya maambukizi ya virusi vya Corona kupungua.
Taarifa ya kuruhusiwa imetolewa hivi punde na Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmood Thabit Kombo (picha juu) na kusema serikali imefikia uwamuzi huo baada ya kujiridhisha na kiasi kidogo cha maambukizi ya korona.
Amesema licha ya serikali kuruhusu shughuli za utalii ziendelee lakini ni vyema shughuli hizo zikaendeshwa kwa kuzingatia tahadhari ya virusi vya corona kwa wageni kupimwa kila wanapoingia nchini na wageni wote kutakiwa kuwa na bima zao za afya kabla hawajaingia nchini. Mgeni au mwenyeji atakaeonekana na maambukizi ya coronavirus basi atapelekwa Kidimni ambako ndiko matibabu hupatikana ya ugonjwa huu.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments :
Post a Comment