Bi Karume ni mmoja ya watu ambao walikuwa ni wakosoaji wakuu wa utawala wa Magufuli nchini Tanzania, alitumia ukurasa wake wa Twitter kueleza fikra zake ambazo mara nyingi zilikuwa ni mwiba kwa mamlaka.
Kupitia mtandao huo pia amekuwa akieleza namna gani hayati Magufuli ama utawala wake ulikuwa kwake.
Muda mfupi baada ya kutolewa kwa tangazo la kifo cha Rais Magufuli alituma ujumbe: "Imekuwa ni miaka mitano ya kuogofya nchini Tanzania lakini nashukuru na kujivunia kuwa nilibaki na utu wangu hata pale ambapo uovu ulitamalaki. Asante nyote ambao mlifanya miaka mitano hii kuvumilika."
Mwisho wa Twitter ujumbe, 1
Na baada ya kukosolewa kwa kuendelea kumkosoa Magufuli hata baada ya kufariki akatuma ujumbe huu: "Alivyokuwa hai, niliambiwa: "Usimseme! Atakudhuru! Ana visasi! Ana power na anaitumia vibaya" Alivyofariki niliambiwa: "Usimseme! Dini, mila na desturi haziruhusu mabaya ya maiti kusemwa" Swali: Kuna watu wako untouchable? Hatuna rukhsa kusema mabaya yao wakiwa hai na wakifariki?"
Mwisho wa Twitter ujumbe, 2
Pia ameeleza kuwa hajafurahia kifo cha Magufuli kama baadhi ya watu walivyodhania: "…Kuna wale ambao wanaweza kuamini kuwa nilisherehekea niliposikia (taarifa ya ) kifo cha Magufuli lakini ukweli ni kwamba nilihisi "faraja" na "shukrani" kwa uwezekano wa mwanzo mpya."
Mwisho wa Twitter ujumbe, 3
No comments :
Post a Comment