dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, April 4, 2021

ALIEKUWA BALOZI WA TANZANIA NCHINI CANADA BW. ALPHAYO KIDATA AENDELEA KUWASTAAJABISHA WENGI NCHINI!

BWANA ALPHAYO KIDATA AMBAE AMEREJEA TENA KUWA  
KAMISHNA MKUU WA MAPATO (TRA)

Bwana
Alphayo Kidata anaweza kuwa ni mtu pekee katika Serikali ya Awamu ya 5/6 ambaye ameweza kushika nafasi zaidi ya nne muhimu katika muda mchache tangu mwaka 2015.

Akitoka kuwa Katibu Mkuu wa Ardhi, Nyumba na Makaazi na kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato, baadae akawa Katibu Mkuu Ikulu na pia akawa Balozi wa Tanzania nchini Canada na mpaka jana alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara tangu Septemba 20, 2019.

Leo Bwana Alphayo Kidata ambae alivuliwa title ya ubalozi baada ya kutumbuliwa kama balozi wa Tanzania nchini Canada amerejeshwa tena kwenye Mamlaka ya Mapato - hii nayo itakuwa ni mara ya kwanza kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato kurejea tena kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka hio.


Marehemu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Alphayo Kidata kuwa balozi wa Tanzania nchini Canada kwenye hafla ndogo iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 10, 2018.


ZACADIA (Zanzibar-Canadian Diaspora Association) ilishiriki sherehe ya kumkaribisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada tarehe 18 August, 2018 mjini Ottawa. Pichani juu kutoka kushoto anaonekana Rais wa Zacadia Shk Omar Ali, akifuatiwa na Balozi mpya H.E Alphayo J. Kidata, baadae anaonekana Bi Shahida Hamad (mjumbe wa Kamati Kuu ya Zacadia) akifuatiwa na Watanzania wengine waliohudhuria sherehe hio mjini Ottawa. 





No comments :

Post a Comment