dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, August 7, 2021

Rais Samia ateua viongozi!

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwemo, Athumani Mbuttuka kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali. 

Uteuzi huo umefanywa jana Ijumaa, tarehe 6 Agosti 2021. Teuzi zote zimeanza 5 Agosti, 2021.

Taarifa iliyotolewa na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu imesema, Mbuttuka anachukua nafasi ya Balozi Mohamed Mtonga ambaye amestaafu na Balozi wa Tanzania katika Falme za Kiarabu (UAE).

Kabla ya uteuzi huo, Mbuttuka alikuwa Msajili wa Hazina.

Pia, Rais Samia amemteua Leonard John Mkude kuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali. Mkude anachukua nafasi ya Francis Mwakapalila ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Kabla ya uteuzi, Mkude alikuwa Meneja Bajeti, Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Rais Samia amemteua Mgonya Benedict kuwa Msajili wa Hazina. Benedict anachukua nafasi ya Athumani Mbuttuka ambaye ameteuliwa kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali.

Kabla ya uteuzi huo, Benedict alikuwa Meneja wa Masuala ya Fedha na Madeni, Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Taarifa imesema, Rais Samia amemteua Frank Mugeta Nyabundege kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo.

Kabla ya uteuzi huo, Nyabundege alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Lake Oil Tanzania Limited.

Pia, amemteua Casmir Kyuki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTT – AMIS. Kyuki ni Katibu wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.

No comments :

Post a Comment