Akihutubia Taifa la Kenya leo July 05,2024 Ruto ametangaza kupunguza idadi ya Washauri wake kwa 50% ambapo ameanzisha hatua nyingine kadhaa za kubana matumizi ili kupunguza gharama kubwa ambazo Serikali inaingia na pia amekata bajeti za ukarabati wa majengo ya Serikali kwa 50%.
Ruto pia amesema hakuna Afisa wa Serikali atakayeruhusiwa kushiriki katika shughuli za kuchangisha pesa zinazoendelea na amewaagiza Maafisa wa Serikali kuacha shughuli za hisani, hasa walioonekana wakionyesha pesa nyingi wakati wa hafla za kutoa misaada ambayo imezua taharuki kutoka kwa Wakenya.
Ruto amesema kufuatia mashauriano mapana na wenzake wameafikiana kupunguza gharama mbalimbali zikiwemo kufuta angalau Mashirika 47 ya Serikali yenye vipengele vinavyoingiliana lengo likiwa ni kuboresha huduma za Serikali kwa Wananchi na kuwafanya Wakenya wapate huduma sahihi kutoka Serikalini.
No comments :
Post a Comment