Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, January 16, 2013

GESI YA MTWARA: JK akemea wanasiasa kuhusu rasilimali

NA MWANDISHI WETU

16th January 2013

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Rais Jakaya Kikwete amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kutumia suala la rasilimali za taifa, ikiwamo gesi asilia kujitafutiaumaarufu wa kisiasa na kuwapotosha wananchi.

Alisema kuwa ni jambo la hatari na lisilo na tija kwa wanasiasa kujaribu kuigawa nchi vipande vipande kwa sababu ya kujitafutia umaarufu kwa kutumia rasilimali za taifa.
 Rais Kikwete aliyasema hayo jana alipokutana na Balozi wa Uingereza nchini ambaye anamaliza muda wake, Dianne Corner.

Kuhusu ugunduzi wa gesi asilia uliofanywa na Kampuni BG ya Uingereza katika eneo la Msimbati kwenye Bahari ya Hindi, walikubaliana kuwa hilo ni jambo jema na lenye kuleta matumaini kwa Tanzania. 

Rais Kikwete alisema kuwa ni tabia ya hatari kwa wanasiasa kutumia gesi asilia hiyo ama rasilimali nyingine kujijengea umaarufu.

“Unawezaje kuwa na nchi moja na taifa moja wakati kila mmoja anadai rasilimali kutoka kwenye eneo moja ibakie na kunufaisha watu wa eneo hilo tu. Huwezi kuwa na nchi moja na yenye umoja wakati kuna nchi ya gesi asilia kule Mtwara, kuna nchi ya kahawa kule Kilimanjaro, kuna nchi ya chai na ndizi kule Bukoba,”

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais  Ikulu ilimkariri Rais Kikwete akisema.

“Kwa sababu kama gesi asilia inatakiwa kubakia na kunufaisha watu wa Mtwara tu, basi wenye haki zaidi ya kudai jambo hili siyo watu wa Mtwara bali ni watu wa Msimbati ambako ndiko ilipogunduliwa gesi ambako ni maili 60 kutoka Mtwara, kilomita 200 kutoka Newala,” aliongeza.


CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment