
Haya haya wazanzibari! Kumekucha! La mgambo likilia kuna jambo! Chama cha wananchi CUF kinawatangazia wanachama, wapenzi na wazanzibari wote wa mikoa miwili ya Pemba, wazalendo na wapenda nchi yao kwa jumla kuhudhuria kwa wingi katika mkutano mkubwa wa hadhara wa aina yake utakaofanyika leo Jumamosi tarehe 16/03/2013 katika viwanja vya Tibirinzi, Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba. Mgeni rasmi katika Mkutano huo ni Simba wa nyika, tishio la vibaraka wauza nchi yetu, kipenzi cha wazanzibari, mwenye uzalendo wa hali ya juu na mapenzi makubwa kwa Zanzibar na wazanzibari, Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Agenda kuu katika mkutano ni kwa nini wazanzibari wanataka mamlaka kamili ya nchi yao? ni jinsi gani wazanzibari wanavyopaswa kujipanga kuelekea kuitia mikononi mwao Zanzibar yao yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa? Kwa nini muungano wa MKATABA na Tanganyika badala muungano wa kinafiki uliopo sasa hauepukiki?.
Halkadhalika hali ya kisiasa na madudu yanayojiri nchini wakati huu wa mpito kuelekea Zanzibar mpya yatazungumzwa na kufafanuliwa. Mkutano utaanza saa 8 barabara za mchana hadi saa 12:00 jioni.
Hatumwi motto! Shime wazanzibari wote kuhudhuria kwa wingi bila ya kukosa!
TUNATAKA NCHI YETU SASA TUMECHOKA TAFRANI!
HAKI!
Chanzo: Mzalendo
No comments :
Post a Comment