zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, March 13, 2013

Wateja wafurika benki Dar

NA JIMMY MFURU

13th March 2013


Mkurugenzi wa Huduma za Kibenki kutoka BoT, Emmanuel Boaz
Zikiwa zimebakia siku mbili kwa wateja wa benki nchini kuhakiki taarifa za akaunti zao, benki kadhaa zimekumbwa na msongamano mkubwa jijini Dar es Salaam.

NIPASHE jana ilishuhudia wateja mbalimbali wakichukua fomu na wengine kurejesha kwa ajili ya zoezi la uhakiki katika benki za NMB,CRDB, NBC na Azania kabla ya kufungiwa akaunti zao kama hawatatekeleza zoezi hilo ifikapo keshokutwa.

Zoezi hilo ambalo lilitakiwa kukamilika mwaka jana mwanzoni, lakini kutokana na wateja wengi kushindwa kuhakikia taarifa za akaunti zao, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) liliongeza mwaka mmoja  ambao utamalizika keshokutwa.

Akizungumza na NIPASHE kwa masharti ya kutotajwa jina lake gazetini, mhudumu wa benki ya CRDB tawi la Azikiwe, alisema wateja walijitokeza siku chache zilizopita.

Alisema tangu zoezi hilo liongezewe muda ni wateja wachache waliojitokeza, lakini kwa sasa wamekuwa wengi kuhofia kufungiwa akaunti zao kutokana na agizo lililotolewa na BoT.

Hata hivyo, baadhi ya wateja walionekana kutokuwa na viambatanisho vinavyotakiwa na  kurudishwa na wahudumu wa benki kwa ajili ya kuwasilisha vinavyotakiwa.


CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment