AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, June 28, 2013

Bajeti ofisi ya Maalim Seif yakwama

NA MWINYI SADALLAH

28th June 2013


Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad
Hofu ya kutopatikana tija kwa fedha nyingi zinazoidhinishwa katika bajeti kwa ajili ya miradi ya kupambana na ukimwi imesababisha makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, kukwama kupitishwa.

Makadirio ya matumizi ya ofisi hiyo yalikwama kupitishwa juzi jioni baada ya Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Jimbo la Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu kuzuia shilingi katika fungu la uratibu na utawala lililopangiwa kupata Sh. 768,000,000.

Kati ya fedha hizo, mwakilishi huyo alitaka Sh. milioni 270 zikatwe na kupelekwa kwenye shughuli za kudhibiti uharibifu wa mazingira, kupambana na dawa za kulevya na kusaidia watu wenye ulemavu.

Jussa alitoa hoja hiyo wakati Baraza lilipokaa kama kamati ya matumizi kupitisha vifungu vya makadirio ya bajeti ya ofisi hiyo, ambapo alisema eneo hilo linapatiwa fedha nyingi lakini tija inayopatikana hailingani na thamani ya fedha hizo.

Alisema mwaka ujao wa fedha Tume ya Ukimwi imepanga kutumia Sh. bilioni 3.5 zikiwemo fedha kutoka kwa washirika wa maendeleo wakati kiwango cha maambukizi ya virusi vya ukimwi kimeongezeka pamoja na tume hiyo kupatiwa fedha nyingi katika mwaka wa fedha unaomalizika.

Jussa alisema kama serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kampeni ya kuzuia maambukizi lakini tija inayopatikana hailingani na thamani halisi ya fedha hizo, ni vizuri zikapelekwa kwenye maeneo ambayo ofisi yenyewe imekiri inakwama kutekeleza.

Mwakilishi wa Kiwani, Hija Hassan Hija naye alitaka maelezo kuhusu mgao mdogo wa bajeti unaopewa shughuli za hifadhi ya mazingira eneo ambalo alisema linapigiwa kelele dunia nzima.

Alisema bajeti ya Idara ya Mazingira imekuwa ikikosa fedha kulingana na mahitaji yake halisi na hivyo kusababisha kukwama kwa miradi mingi ya vikundi vinavyoshughulikia hifadhi ya mazingira kwenye maeneo yanayoathirika kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment