Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, October 9, 2013

SHAKA: ‘NITAWATAJA WANAOTOA VYETI KISIASA’

Written by   //  08/10/2013 

Na Mwandishi wetu
NAIBU Katibu Mkuu umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Shaka Hamdu Shaka amesema atawataja watendaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) Idara ya nyaraka,  vizazi na vifo wanaotoa vyeti vya kuzaliwa kwa mwelekeo wa kisiasa.
Kiongozi huyo umedai kwamba wafanyakazi wanaofanya hivyo wanalenga kuwapatia  vitambulisho vya ‘Mzanzibari Mkaazi’, jamaa na ndugu zao wasio na sifa kwa lengo maalum.
Akihutubia mkutano wa hadhara juzi kwenye Uwanja wa Garagara, Jimbo la Mtoni Unguja, Shaka alisema baadhi ya wafanyakazi wa Idara hiyo wanakiuka utaratibu wa  kazi.
Alisema kwamba kuwapa watu wasio na sifa vyeti vya kuzaliwa ni kinyume na utaratibu wa sheria na ni kosa. Kiongozi huyo wa UVCCM, Zanzibar alisema anao ushahidi wa madai yake hayo.
Alisema wafanyakazi hao wanashabiki siasa kwa kuwapa watu vyeti vya kuzaliwa, hatua itakayo wasaidia kupata vitambulisho vya ukaazi, na kuweza kuandikishwa katika daftari la  kudumu la wapiga kura.
Shaka alisema Idara hiyo ipo chini ya Wizara ya Katiba  na Sheria, inayoongozwa na Waziri Abubakar Khamis Bakar kutoka Chama cha Wananchi (CUF).
Alisema Idaya hiyo imeajiri wafanyakazi wapya na kuwahamisha wa zamani ili kupata  mwanya wa kufanya upendeleo kwa mtazamo wa kisiasa:
“Tunayo majina ya wafanayakazi wa Idara hiyo wanaofanya mchezo  huo mchafu,  wasipojirekebisha tangu sasa tutawataja majina yao,” alisema Shaka na kuongeza:
“Tunaitaka Wizara ya Katiba  na Sheria ichukue hatua zinazostahili kuzuia mpango wa siri unaolenga kuleta  vurugu na  upendeleo,”.
Shaka, pia alimwambia Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif  Sharif Hamad kuacha kudhihaki Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.
Alisema Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif anaimba nyimbo kwenye  majukwaa huku  vitendo na matamshi yake hayaheshimu na kuyaenzi  Mapinduzi hayo.
Naye, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi wa CCM Zanzibar, Najma Murtaza Giga  aliwaasa viongozi wa vyama vya upinzani kuachana na dhana kwamba CCM imechoka  kiakili na wanaweza kuiburuza.
Chanzo: Mzalendo

No comments :

Post a Comment