Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 19, 2013

Uholanzi yatoa Sh.bilioni 66 kusaidia umeme nchini

NA WAANDISHI WETU

19th October 2013
Chapa
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO), Sophia Mgonja (Kulia), akibadilishana hati na Mkurugenzi wa Mauzo, wa kampuni ya utengenezaji jenereta za umeme ya Uholanzi, Zwart Tecgniek, Paul Van der Weiden, mara baada ya kutiliana saini makubaliano kujenga jenereta za umeme kwenye wilaya za Mpanda, Ngara na Biharamulo. Mkataba huo wenye thamani ya Euro milioni 33, zilizotolewa na Tanzania asilimia 50 na Uholanzi asilimia 50 utakaomilika katika kipindi kifupi kijacho. Wanaoshuhudia, ni mwenyekiti wa bodi ya Tanesco, Jenerali (Mstaafu), Robert Mboma (Wakwanza kulia), Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi (Watatu kulia) na balozi wa Uholanzi nchini Jaap Frederiks. (Watano kulia). (Picha na Khalfan Said)
Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) na Kampuni ya uzalishaji umeme ya Zwart Techniek ya Uholanzi, zimetiliana saini ya kuanzisha mradi wa umeme katika mikoa ya Kagera na Rukwa utakaogharimu Sh.bilioni 66.

Mradi huo utazalisha umeme wa megawati 7.5 katika wilaya za Ngara, Biharamulo (Kagera) na Mpanda (Rukwa), ujenzi unaotarajiwa kuanza mwezi Novemba, mwaka huu.

Akizungumza  wakati wa uwekaji saini jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, alisema kuanzishwa kwa kituo hicho ni moja ya mikakati ya serikali iliyoahidi kupambana na tatizo la umeme nchini hususani mikoa ambayo haina umeme wa uhakika na vijijini.
Maswi alisema kwa sasa serikali ina mpango wa kupeleka umeme katika mikoa ya Ruvuma na Njombe ambayo haina gridi ya taifa hususani Songea na Makambako, na mkataba unatarajiwa kufanyika mwezi huu.

“Shirika letu la umeme limejipanga kusambaza umeme kwenye mikoa yote na hivi sasa mikoa ya Lindi na Mtwara tayari imefikiwa hivyo hakuna mkoa utakaoachwa kwenye mpango huu na matokeo makubwa sasa,” alisema Maswi.

Aliongeza kuwa fedha za mradi huo zitachangiwa na serikali zote mbili za Tanzania ambayo imetoa asilimia 50 na Uholanzi asilimia 50.

Kwa upande wake, balozi wa Uholanzi nchini, Jaap Fredriks, alisema urafiki wa Uholanzi na Tanzania ulianza muda mrefu na utaendelea kudumu, na kueleza kuwa mradi huo wa ufuaji umeme utaleta manufaa kwa nchi zote mbili sio Tanzania peke yake.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment