AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, November 4, 2013

Malalamiko Tanzania, Burundi kuhusu EAC kujadiliwa Nov. 28

NA JOHN NGUNGE

4th November 2013


Dk.Richard Sezibera
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Balozi Dk. Richard Sezibera, amesema malalamiko yaliyotolewa na Tanzania na Burundi kuhusu kuwekwa pembeni na nchi nyingine wanachama katika Mkutano wa 19 wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki, yanafanyiwa kazi.

Katika taarifa yake fupi kwa vyombo vya habari  iliyotolewa mwishoni mwa wiki kuhusu 'Hali ya mambo katika Jumuiya' Dk. Sezibera, alisema malalamiko hayo yatazungumzwa katika kikao cha 28 cha Baraza la Mawaziri kinachotarajiwa kufanyika Novemba 28, mwaka huu. Alisema kikoa hicho kitatoa mapendekezo kwa mkutano mkuu.
Alisema katika moyo wa kujenga na kuimarisha mtangamano wa jumuiya, mawaziri hao wamepeana taarifa kuhusu yaliyojiri kwenye mikutano hiyo na changamoto zilizojitokeza.

Alisema hivi karibuni kumekuwa na taarifa kwenye vyombo vya habari kuhusu mikutano kadhaa ya viongozi wa nchi za Rwanda, Uganda na Kenya iliyokuwa ikifanywa bila kuwashirikisa marais wa Tanzania na Burundi.

Alisema nchi wanachama zimekubaliana kutekeleza mikataba ya soko la pamoja na umoja wa forodha na kuondoa vikwazo katika biashara pamoja na uhuru wa watu kwenda nchi nyingine.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment