AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, November 5, 2013

Serikali kumiliki TTCL kwa asilimia 100

NA MWANDISHI WETU

4th November 2013


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kulia), akizungumza na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mawasilino Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto), wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa kampuni hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wa pili kushoto ni Ofisa Mkuu Ufundi wa TTCL, Jotham Lujara na Mkurugenzi Rasilimali Watu TTCL, Edward Emmanuel.
Serikali imesema inaendelea na mchakato wa majadiliano na Kampuni ya Simu za Mikononi ya Airtel kuiwezesha serikali kumiliki hisa zote za Kampuni ya Mawasiliano ya (TTCL).

Naibu wa Waziri, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba alisema hayo wakati akifunga kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa TTCL jijini Dar es Salaam.

Alisema ni nia ya serikali kuona inamiliki TTCL kwa asilimia 100.

“Kwa sasa shirika hili lina miundombinu yote na uwezo wa kufanya kazi vyema,” alisema. Kwa sasa kampuni ya Airtel inamiliki asilimia 65 wakati TTCL inamiliki asilimia 35.

Aliongeza kusema kuwa ni dhamira ya wizara na serikali kuona TTCL inashika hatamu katika kuongoza sekta ya mawasiliano hapa nchini ili kufikisha huduma hiyo sehemu zote za nchi.

Aliitaka kampuni hiyo kuingia katika teknolojia ya masafa ya GSM ambayo yanawezesha wateja kutumia simu moja kwa laini zaidi ya moja tofauti na teknolojia inayotumika sasa ya CDMA ambayo inatumia laini moja tu.

Alisisitiza kwamba serikali itaiwezesha kampuni kupata mkopo kwa ajili ya kufikia malengo yake hayo ili kuzidi kutoa huduma bora kwa Watanzania.

Pia alipongeza kampuni hiyo kwa kutoa huduma bora ya mkongo na aliagiza uongozi kuzidi kuutunza na kutafuta masoko zaidi ili watu wazidi kupata huduma za mawasiliano yakiwamo ya intaneti kwa ufanisi na urahisi.

CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment