Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, November 13, 2014

MZEE MAJUTO ATUJIA JUU ZANZIBAR NI KWETU!

  • ATUPIGIA SIMU ZANZIBAR ETI KUTUSUTA KUWA HAJAFA BADO!
  • ATUTISHIA KAMA TUNAZIWEZA TUMFUATE DSM!
Mzee Majuto anaonekana akiongea na Zanzibar Ni Kwetu jana jioni kutoka kwake mjini Dar-Es-Salaam!

Jana blog letu la Zanzibar Ni Kwetu liliripoti juu ya muvi mpya ya yule msanii mkongwe na machachari wa hapa nchini Tanzania ajulikanae kama Mzee Majuto. Muvi hio ambayo tayari ipo madukani ali-act yeye na Bi Chau. Katika muvi hii (kwa wale ambao bado hawajaiona) Mzee Majuto anakufa ghafla ofisini kwake mjini DSM kutokana na kusikia kuwa Bi Chau kafariki baada ya ajali mbaya iliyotokea huko Sinza wakati akielekea kwao Nyanjati.

Ni kweli kabisa jamani kuwa kila mtu hapendi kufa, hata akiwa ameshakula chumvi kiasi gani, kwasababu hatufahamu kwanini Mzee Majuto akaacha kazi zake muhimu na akatupigia simu Zanzibar na huku akifoka kama vile tumemtabiria kifo cha kweli mzee wetu mpenzi, wakati yeye mwenyewe ndio aliyoiandika hio script ya muvi yake.

Tunahakika kuwa hakuna atakaeamini hii habari ifuatayo, ambayo labda ingelipata kichwa cha maneno kama vile - A fatal head-on collision with King Majuto!

Ilikuwa saa tisa na dakika kama tano hivi ya jioni hio jana (Wednesday) wakati simu ilivyolia. Kupokelewa Mzee Majuta  kwa sauti ya juu akauliza hata bila ya salaam kuwa ni nani huyu Zanzibar Ni Kwetu? Aliepokea simu akamuuliza, “ kwani wewe mwenzetu ni nani na unamtaka nani?”. Akasema mimi ni Amri Athumani au kwa jina jengine Majuto. Kusikia hivyo aliepokea simu akajua  kuwa sasa trouble is on the way na mbio mbio akaipeleka simu kwa Mkuu wa Mawasiliano wa Zanzibar Ni Kwetu, ambae akamuuliza mzee Majuto baada ya kumuamkia “ tukusaidie nini King Majuto?”.

Mzee wetu Majuto akajibu kwa ghadhabu kubwa sana, “sina haja ya shikamoo zenu, kwasababu nyinyi ni wauwaji”, na akaendelea kumuuliza tena Mkuu wa Mawasiliano, “ni nani huyu Zanzibar Ni Kwetu?”. Akajibiwa kuwa huyu sio mtu bali ni blog.

Mzee Majuto akaulizwa umeipata vipi nambari ya simu wakati haipo kwenye blog? Majuto akajibu, kwani mimi sijui ku-guguli?”

Akaendelea mzee Majuto…” Kwanini  mnanitakia kifo? Hata wife wangu alishituka alipoona kichwa chenu cha habari kuwa MAJUTO AMERFARIKI GHAFLA kwenye hilo bologu lenu na mpaka sasa yupo kwenye mshituko bado. Basi mjue mtatangulia nyinyi kwanza mbele ya haki!”. Akaulizwa, "kwani mzee Majuto kwenye hii muvi yako ya sasa sio ume-act kama ulikufa au vipi? Sasa sisi tulichoripoti kwa wasomaji wetu ni hicho tu bila ya kuengeza kitu zaidi".

Akaruka mzee Majuto, “ kwanini mmeigeuza hali kama vile kweli nilikufa wakati ilikuwa ni kwenye muvi tu? Mnajua simu ngapi nilipigiwa leo na wapenzi wangu wakiniulizia? Siku yangu ya leo yote mmeiharibu”. Akajibiwa kuwa, “kufa ni kufa tu mzee Majuto, kama kwenye mchezo au nje ya mchezo. Uki-act umekufa itabidi tuandike hivyo hivyo. Vyenginevyo usi-act umekufa. Sasa ulitaka tueleze kuwa kwenye hii muvi yako ulikuwa hujafa ghafla kutokana na mapenzi yako juu ya Bi Chau?”.

Maneno hayo inaonesha yalimkera sana mzee Majuto na ghafla akaruka, “Sikilizeni nyinyi watoto wa hilo bologu la Zanzibar Ni Kwetu, nyinyi sasa najua kuwa mlikusudia ugomvi na mimi, lakini kama mnaziweza basi njooni Dalesalama wakati wowote ule na hata nikiwa usingizini hamtonishinda mimi”, akamalizia mzee Majuto.

Mzee Majuto akaelezwa kuwa hakuna ugomvi na wala hapajakusudiwa shari na kama anahisi hivyo basi anaombwa radhi. Mwisho mzee Majuto akaulizwa, “ je, tunaweza kupata discount ya bei ya video cassette moja kwaajili ya maktaba yetu?” Mzee Majuto akaruka kwa sauti kali na kusema, “kwa nyinyi Zanzibar Ni Kwetu bei ni laki moja” na akaikata simu hapo hapo!

Pia soma: http://zanzibarnikwetu.blogspot.ca/2014/11/mzee-majuto-kifo-chake-cha-ghafla.html

No comments :

Post a Comment