Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, February 15, 2016

20 jela kwa kushindwa kusafisha mazingira


By Mussa Mwangoka, Mwananchi 
Sumbawanga. Wakazi 20 wa kata za Kirando na Mkinga wilayani Nkasi Mkoa wa Rukwa, wamehukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela au kulipa faini ya Sh20,000 kila mmoja kwa kushindwa kusafisha mazingira na kuchimba vyoo ili kudhibiti kipindupindu.
Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo, Chala Wilgis Mbunda alitoa hukumu hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita.
Alisema kwa mujibu wa Sheria ya Afya ya Mwaka 2009, Kifungu cha 53,54,55 (C) na 111 (1) (2), watalipa faini hiyo na kuchimba vyoo ndani ya siku saba tangu wahukumiwe.
Wakati huohuo; watu wengine 15 wamehukumiwa kulipa faini ya Sh30,000 au jela miezi mitatu kila mmoja kwa kosa la kuacha kuchimbva mashimo ya taka na vichanja.
Hata hivyo, watuhumiwa hao walilipa faini huku wengine wawili wakihukumiwa kuchapwa viboko baada ya umri wao kuwa chini ya miaka 18.
Hivi karibuni ugonjwa huo ulilipuka miezi kadhaa iliyopita katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika na kuua watu zaidi ya 10.
Eneo hilo limekuwa likikumbwa na maradhi hayo, kutokana na jamii ya watu wake kutokuwa na utamaduni wa kutokuwa na vyoo bora.
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Iddy Kimanta alinukuliwa hivi karibuni akisema Serikali imejikita kuhakikisha kila kaya inakuwa na choo bora sambamba na matumizi sahihi ya vyoo hivyo.

No comments :

Post a Comment