Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, February 18, 2016

Prof. Mbarawa azishukia Temesa, TTCL.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, ameelezea kutoridhishwa kwake na utendaji      kazi  wa  Wakala wa Umeme na Ufundi (Temesa) juu ya uendeshaji wa vivuko na ukusanyaji mapato.
 
Sambamba na hilo, ameitaka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kubadilika kiutendaji ili kujiendesha kibiashara badala ya kutegemea serikali.  
 
Akizungumza jana na wafanyakazi wa wizara hiyo mjini hapa, Profesa Mbarawa, alisema serikali itachukua uamuzi mgumu ikiwamo kuwachukulia hatua wale wanaoshindwa kuwajibika. 
 
Alisema wizara ilitangaza kutumia Sh. bilioni 60 kufanya matengenezo na ukarabati mkubwa wa uwanja wa ndege wa Musoma ili kuwaondolea adha wananchi wa mkoa na watalii wanaofika kutembelea hifadhi ya taifa ya Serengeti.
 
Alisema hatua  hiyo  inalenga  kumuenzi Baba wa Taifa  Hayati  Mwalimu Julius Nyerere, hivyo  serikali imetenga dola milioni 30 (zaidi ya Sh. bilioni 60 kwa ajili ya kazi hiyo.Aliongeza ulegevu katika kazi umesababisha  adha kubwa  kwa   wananchi  ambao   sasa   wanalazimika kusafiri   hadi   mkoani   Mwanza  kutafuta huduma  hiyo  huku   uwanja  huo  ukikosa mapato. 
 
Kuhusu   Kampuni  ya Simu  Tanzania (TTCL), Profesa Mbarawa alisema inapaswa kubadilika kiutendaji badala ya kutegemea serikali kufanya biashara ili kuongeza pato la taifa. 
 
Hivi karibuni, Profesa Mbarawa alianza kazi ya kusafisha taasisi Zilizo chini ya wizara yake kwa kuwang’oa vigogo waandamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (THA) na kuwahamishia makao makuu ya wizara. Pia alimsimamisha kazi meneja wa Fedha wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kwa ubadhirifu wa mamilioni ya fedha.   
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment