dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, April 14, 2016

RAIS MAGUFULI AKATAZA WAKURUGENZI KWENDA NA MASHANGINGI DODOMA...SASA KWENDA NA COASTER


Rais John Pombe Magufuli ameagiza kuwa Wakurugenzi wote wa Wizara mbalimbali watakaohudhuria vikao vya kamati za bunge Mjini Dodoma, watasafiri kwa mabasi badala ya magari yao "mashangingi" ya serikali kama ilivyozoeleka.

Katika utaratibu huo mpya kila Wizara itakodi basi (Coaster) kwa ajili ya kusafirisha Wakurugenzi hao kwenda Dodoma kwenye vikao vya bunge ili kutoa msaada kwa wizara zao pale wanapohitajika kufanya hivyo. Rais amefikia maamuzi haya ktk jitihada za kupunguza gharama za mafuta na posho za madereva wa wakurugenzi wanaposafiri kuelekea Dodoma.

Hata hivyo Wakurugenzi hao hawazuiwi kusafiri kwa magari yao binafsi (personal) kwa kujilipia gharama zote wao wenyewe ikiwa watataka kufanya hivyo. Katika utaratibu huu mpya inamaanisha kuwa viongozi wa wizara watakaosafiri kwa "mashangingi" kuelekea Dodoma ni Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu mkuu tu.

No comments :

Post a Comment