dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, April 13, 2016

WAGOMBEA NASAFI YA KATIBU MKUU UMOJA WA MATAIFA WAANZA KUHOJIWA

Mgombea wa Nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Igor Luksic ( Montenegro), akimwaga sera zake mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, wakati wa majadiliano/mhadalo usio rasmi ulioandaliwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa lengo kutoa fursa kwa wanaowania nafasi ya Katibu mkuu kueleza sera zao na kisha kuulizwa maswali
Bi. Irina Bokova ( Burgalia) mmoja wa wanawake wanne waliojitokeza hadi sasa kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa naye akijieleza mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Bw. Antonio Guterres ( Portugal) mmoja wa wagombea waliohojiwa katika siku ya kwanza ya mdahalo usio rasmi wa kuwasikiliza wagombea waliojitokeza kuwaania nafasi itakayoachwa wazi na Ban Ki Moon, mwishoni mwa mwaka huu. jumla ya wagombe tisa wamekwisha jitokeza mpaka jana ( jumanne)
Taswira ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, katika siku ya kwanza ya mdahalo wa kihistoria ya wagombea nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mdahalo/majadiliano ya kwanza ya aina yake kufanyika katika nafasi ya kumtafuta Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Na Mwandishi Maalum, New York
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, jana ( Jumanne) limeandika historia kwa mara nyingine, kwa kuanza mchakato usio rasmi wa kuwasikiliza na kuwauliza maswali wagombea watarajiwa waliojitokeza kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Mchakato huo ulianza kwa kuwasikiliza wagombea watatu kati ya tisa wakiwamo wanawake wake wanne ambao hadi siku ya jumanne walikuwa wametangazwa rasmi kuwania nafasi hiyo itakayo achwa wazi na Katibu Mkuu wa sasa Ban Ki Moon anayemaliza muda wake mwishoni mwa mwaka huu.Katika awamu ya hiyo ya kwanza, kila mgombea mtarajiwa alipewa fursa ya kujieleza na kuelezea visheni yake, sera, mipango, vipaumbele vyake na nini anatarajia kukifanya endapo atachaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa , Umoja wenye wanachama 193.

Walioshiriki mdahalo huo katika siku ya kwanza walikuwa ni Dr. Igor Luksic ( Motenegro), Bi. Irina Bokova ( Bulgaria) na Bw. Antonio Guterres ( Portugal)

Wengine ambao wamejitokea kuwania nafasi hiyo ni Dr. Damilo Turk ( Slovenia) Prof.Dr. Vesna Pusic ( Crotia), Bi. Natalia Gherman ( Moldova), Dr. Srgian Kerim ( Macedonia), Bi. Helen Clark ( New Zeland) na Bw. Vuk Jeremic ( Serbia)

Ulikuwa ni mdahalo wa aina yake wa kwanza kutokea tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa miaka karibu 70 iliyopita, mdahalo ulioendedeshwa katika mazingira ya uwazi, na ambao kwayo umebadilisha kabisa utaratibu wa kumpata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Mdahalo huo ambao umeratibiwa na kusimamiwa na Rais wa Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa Bw. Monges Lykketoft, umetokana na makubaliano ya pamoja kati ya Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, na Rais wa Baraza la Usalama wakati huo ( mwezi desemba) Mwakilishi wa Kudumu wa Marekani. Na pia azimio namba 69/321 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Katika barua yao kwa wawakilishi wa kudumu wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, Bw. Lykketoft na Balozi Samantha Power ( USA) walieleza juu ya kuwapo kwa majadiliano au mdahalo wa wazi na usio rasmi lakini muhimu ambapo makundi yote yanayowakilisha nchi wanachama wa UN yatapata fursa ya kuwauliza maswali wagombea, maswali ambayo yamejielekeza zaidi kwa maslahi ya makundi hayo, vipa umbele vyao na namna wanavyouona Umoja wa Mataifa katika sura yake ya sasa.

Kama ilivyoelezwa hapo awali, hii ni mara ya kwanza kwa historia ya Umoja wa Mataifa, kwanza, kutoa fursa kwa wagombea wengi kujitokeza kuwania nafasi hiyo na kupewa nafasi ya kujieleza, pili nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kupewa fursa ya kuwafahamu, kuwasikiliza na kisha kuwauliza na maswali, na tatu Asasi zisizo za kiserikali nazo kushirikishwa katika mchakao huu.

Vile vile ni historia ya aina yake ambapo kipaumbele kimetolewa kwa wagombea wanawake nao kujitokeza kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa katika Umoja wa Mataifa. Kwa takribani mwaka mmoja sasa kumekuwapo na kundi maalum ambalo lenye limejipambanua kama marafiki wa mgombea mwanamke

Mfumo wa uulizwaji wa maswali kwa wagombea hao ulikuwa ni ule ambao Wenyeviti wa Makundi ya Nchi wa wanachama wa Umoja wa Mataifa kwa mwezi huu wa Nne (April ) ndio waliouliza maswali kwa niaba ya makundi hayo. Aidha hata zile nchi ambazo ni za visiwa au ambazo kwa lugha nyepezi zimezungukwa na mataifa mengine ( land Locked countries) nazo zilipata fursa ya kuuliza maswali yenye maslahi kwa nchi zao.

Kwa mfano maswali ya nchi za Afrika yaliulizwa na Mwakilishi wa Kudumu wa Uganda ambaye ni Mwenyekiti wa Kundi la Nchi za Afrika kwa mwezi huu wa Nne.

Maswali mengi waliyoulizwa wagombea, yamejikita katika maeneo mtambuka kama vile haki za binadamu, operesheni za ulinzi wa Amani na utafutaji suluhu na ufumbuzi wa migogoro, unyanyasaji wa kijisia unaofanywa na walinda Amani, kuimbuka kwa tatizo la ugaidi, tatizo la wakimbizi, utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu ( Agenda 2030), nafasi za uteuzi kwa kuzingatia uwiano wa kijiografia na kikanda katika ngazi za juu za watendaji katika sekretarieti ya Umoja wa Mataifa.

Maswali mengine yalihusu umalizwaji wa ukoloni, utegemezi kwa wafadhili wachache katika uendeshaji wa Umoja wa Mataifa, marekebisho ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yakiwamo kuongezwa kwa idadi ya wajumbe wa kudumu wa baraza hilo, weledi na sifa za uongozi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, na nini kifanyike ili kuufanya Umoja wa Mataifa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kwa kuzingatia mazingira na hali ya sasa na hususani kile kinachoelezwa kupoteza mweleko wa chombo hicho kikiuu cha kimataifa.

Utaratibu uliozoeleka wa uchaguzi au uteuzi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ulibebwa zaidi na matakwa ya Baraza la Usalama na hasa kundi la P5 ambao ni wajumbe wa kudumu wa Baraza hilo katika kupitisha jina la waliyemtaka kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Baada ya Baraza la Usalama, kupitisha jina la mteule waliyemtaka jina hilo baadaye lilipelekwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambalo lilipitisha na halikuwa na uwezo wa kulikataa kwa kuwa limeshapitishwa na Baraza la Usalama.

Utaratibu huu umekuwa ukilalamikiwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lenye wajumbe 193 kwamba lilikuwa likitumikia kutia muhuli jina ambalo limependekewa na wajumbe wachache ( Baraza la Usalama lenye wajumbe 15 wakiwamo watano wa kudumu)

Ni kwa sababu hiyo safari hii Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeamua kuchukua hatamu na baada ya majadiliano ya kina baina ya nchi wanachama kuhakikisha kwamba Baraza hilo linakuwa na kauli au fursa katika uteuzi wa Katibu Mkuu badala ya kuwa watiaji muhuri ( rubber stamp).

Leo (jumatano) itakuwa ni zamu ya Dr. Danilo Turk, Prof.Dr. Vesna Pusic na Bi. Natalia Gherman.

No comments :

Post a Comment