Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema inampango wa kuziondoa skuli za Vikokotoni na Darajani ili kulitumia eneo hilo kwa shughuli za biashara.
Akijibu swali katika kikao cha baraza la wawakilishi Waziri anaeshughulikia serikali za Mitaa Haji Omar Kheri amesema eneo hilo halifai kuweko skuli kutokana na kukosa utulivu.
Amesema skuli hizo zitahamishiwa maeneo ya Rahaleo ili kupisha mpango wa ujenzi wa maduka ya kisasa kufanikisha mpango wa serikali wa kulifanya eneo hilo kuwa la kibiashara.
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imo katika mpango wa kuliendeleza eneo la biashara la Darajan kwa ujenzi wa maduka ya kisasa, bustani za kupumzikia, ujenzi wa ofisi ili kuongeza haiba nzuri ya mji wa Zanzibar.
No comments :
Post a Comment