dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, November 26, 2016

Video:Waziri Mwakyembe amepewa siku 7 kutoa maelezo kwa Waziri Mkuu.!


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amempa siku saba Waziri wa Katiba na Sheria Dr. Harrison Mwakyembe kutoa maelezo ya kwanini Tanzania haijakamilisha mkataba wa mawakili wa Afrika Mashariki, mkataba ambao unafanya kutambuana katika utendaji wao wa kazi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo wakati akimuwakilisha Rais Magufuli katika mkutano wa 21 wa mwaka unaojumuisha chama cha wanasheria wa Afrika Mashariki uliofanyika katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

“Nimeshtushwa kidogo na maelezo kwamba mkataba huu unasubiri tu kusainiwa na wanasheria wakuu wa nchi wanachama, ili uanze kufanya kazi katika nchi zote za jumuiya isipokuwa Tanzania. Natumia nafasi hii kukuagiza waziri uniletee taarifa ofisini kwangu ndani ya wiki moja mnieleze ni kwanini mkataba huu hamkukamilisha kwa kuiingiza Tanzania” – Waziri Mkuu Majaliwa


No comments :

Post a Comment