Watu wasipungua 25 waripotiwa kuuawa katika shambulizi lililtekelezwa katika usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi Magharibi mwa Burundi. Taarifa zizlitolewa na uongozi wa mkoa wa Cibitoke , Magharibi mwa Bunrundi zimefahamisha kuwa wahalifu waliokuwa na silaha wameshambulia mkoani humo na kupelekea watu 25 kufariki.Cibitoke ni mkoa nchini Burundi unaopatikana mpakani mwake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Gavana wa mkoa wa Cibitoke Joseph Iteriteka aliambia shirika la habari la Anadolu la Uturuki kuwa wahalifu hao walishambulia Cibitoke wakitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakiwa na silaha za moto na mapanga.
Watu wanane waliojeruhiwa katika shambulizi hilo walipelekwa mjini Bujumbura kupatiwa matibabu.
Gavana wa mkoa wa Cibitoke Joseph Iteriteka aliambia shirika la habari la Anadolu la Uturuki kuwa wahalifu hao walishambulia Cibitoke wakitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakiwa na silaha za moto na mapanga.
Watu wanane waliojeruhiwa katika shambulizi hilo walipelekwa mjini Bujumbura kupatiwa matibabu.
No comments :
Post a Comment