dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, August 26, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud Akabidhiwa Ripoti ya Maendeleo ya Elimu ya Mkoa wa Mjini Magharibi na Ripoti ya Muelekeo wa Mkakati wa Elimu Kwa Mkoa wa Mjini Magharibi 2018/20191

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud akizindua Ripoti ya Kamati ya Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo kushoto Mwenyekiti wa Kamati hiyo Ndg.Juma Abdallah Hamad, hafla hiyo imefanyika Ofisi za Mkoa Vuga Zanzibar.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud akimpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,Ndg.Juma Abdallah Hamad,baada ya kuizindua, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Afisi ya Mkuu wa Mkoa Vuga Unguja.
MKUU wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud akionesha Ripoti ya Kamati ya Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo kushoto Afisa Tawala wa Mkoa wa Mjini Magharibi Bi. Hamida Mussa Khamis na kushoto Mwenyekiti wa Kamati hiyo Ndg.Juma Abdallah Hamad, hafla hiyo imefanyika Ofisi za Mkoa Vuga Zanzibar.


MKUU wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud akizungumza na kutowa shukrani zake kwa Kamati ya Maendeleo ya kuimarisha Elimu Mkoa wa Mjini Magharibi, kwa kazi nzuri na kupokea matokeo mazuri kwa Wanafunzi wa Kidatu cha Sita katika ufaulo wao katika Mtihani wa Taifa uliofanyika mwaka.
WAJUMBE wa Kamati ya Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa Taarifa ya Ripoti ya Kamati hiyo, hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa Vuga Zanzibar.



No comments :

Post a Comment