Rais wa Iran Hassan Rouhani amesema eneo jipya la machimbo ya mafuta limegunduliwa kusini mwa nchi hiyo, na linakadiriwa kuweza kutoa wastani wa mapipa bilioni 50 ya mafuta ghafi.
Tangazo hilo lilotolewa Jumapili linamaanisha akiba ya mafuta ghafi ya Iran itaongezeka kwa theluthi moja, huku nchi hiyo ikiwa inapambana kuuza mafuta yake nje ya nchi kutokana na vikwazo vya Marekani.
Sekta ya mafuta ya Iran imepata pigo kubwa kutokana na vikwazo vya Marekani, baada ya rais Donald Trump kujitoa katika makubaliano ya mpango unaonekana kusambaratika wa silaha za nyuklia kati ya Iran na nchi nyingine tano zenye nguvu duniani ikiwa ni pamoja na Umoja wa Ulaya.
Rouhani amesema mafuta hayo yamegunduliwa katika eneo lenye utajiri wa mafuta la mkoa wa Khuzestan.
Tangazo hilo lilotolewa Jumapili linamaanisha akiba ya mafuta ghafi ya Iran itaongezeka kwa theluthi moja, huku nchi hiyo ikiwa inapambana kuuza mafuta yake nje ya nchi kutokana na vikwazo vya Marekani.
Sekta ya mafuta ya Iran imepata pigo kubwa kutokana na vikwazo vya Marekani, baada ya rais Donald Trump kujitoa katika makubaliano ya mpango unaonekana kusambaratika wa silaha za nyuklia kati ya Iran na nchi nyingine tano zenye nguvu duniani ikiwa ni pamoja na Umoja wa Ulaya.
Rouhani amesema mafuta hayo yamegunduliwa katika eneo lenye utajiri wa mafuta la mkoa wa Khuzestan.

No comments :
Post a Comment