DK. Bilal Mgeni Rasmi katika Futari Ilioandaliwa na Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ Ltd.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongazana na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Amour, wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana Agosti 8, 2012 kuhudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki hiyo na kufutari pamoja na baadhi ya Waumini wa dini ya Kiislamu walioalikwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Amour, akizungumza machache kuhusu kazi na utendaji wa kazi za Benki hiyo ya Kiislam ya Watu wa Zanzibar (PBZ) na malengo yake wakati wa hafla hiyo ya futari iliyofanyika jana katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
Chanzo: ZANZINEWS (MAPARA)
No comments :
Post a Comment