dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, June 16, 2013

Bomu lalipuka tena Arusha

NA JOHN NGUNGE

16th June 2013


Baadhi ya wakazi wa mji wa Arusha wakiangalia Sehemu waliyokuwepo baadhi ya majeruhi wa mlipuko wa bomu katika mkutano wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi za udiwani jimboni humo jana jioni.
Watu watatu wanasadikiwa kufa katika mkutano wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi za udiwani wa kata nne za Jimbo la Arusha Mjini uliokuwa ukihutubiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe.
Mkutano huo ulifanyika katika viwanja vya Soweto vilivyopo katika kata hiyo na wakati Mbowe akiwa anakaribia kumaliza kufunga kampeni zake, na huku wanachama wakijiandaa kufanya harambee, mtu mmoja ambaye hajafahamika anadaikuwa kurusha bomu kwenye mkusanyiko wa mkutano huo na taarifa za awali zilidai kuwa watu watatu walifariki kutokana na mlipuko huo.

Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, alisema jana kuwa kulitokea mlipuko wa kitu kama bomu lililorushwa na mtu ambaye bado hajafahamika ni nani.
Kufuatia mlipuko huo, polisi waliokuwa wakifanya ulinzi katika mkutano huo, walilipua risasi za moto na inadaiwa kuwa zaidi ya watu 6O hadi 70 walijeruhiwa na kukimbizwa hospitali za Selian na ya Mount Meru.
Tukio hilo limekuja huku maelfu ya wanachama leo wa vyama vya siasa wakipiga kura kuwachagua madiwani wa kata za Kaloleni, Elerai, Kimandolu na Themi.
Hadi NIPASHE JUMAPILI inakwenda mitamboni, Mbowe na viongozi wa mkoa walikuwa wameelekea Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kuwajulia hali watu walioathirika na bomu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Liberatus Sabas, alikuja eneo la tukio lakini hakutaka kuzungumza lolote kuhusu kuhusu mlipuko huo.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments :

Post a Comment