dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, June 22, 2013

Mulugo kufanya ziara za kushtukiza sekondari binafsi

NA MWANDISHI WETU

21st June 2013


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillipo Mulugo
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillipo Mulugo anatarajia kuanza kufanya ziara za kushtukiza katika shule za sekondari binafsi ili kubaini matatizo na migogoro inayozikabili.

Uamuzi huo aliutangaza mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya upanuzi wa  Chuo cha Mtakatifu Augustine Tawi la Mbeya.

Ni baada ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Peter Chacha kumweleza kuwa kushuka kwa kiwango cha elimu kwa shule hizo nchini kunatokana na baadhi ya shule kuwa na migogoro ya kiutawala.

Jaji Chaha alisema kuwa kumekuwa na migogoro katika shule hizo inayosababisha wanafunzi  wengi kufeli katika mitihani yao ya kawaida na ya taifa.

Alisema serikali inatakiwa kufanya uchunguzi katika shule nchini ili kubaini zenye migogoro katika utawala wake.
Alisema kumekuwa na shule ambazo utawala wake umekuwa ukigombania madaraka na kuacha kumpa haki mtoto ya kumfundisha.

“Shule nyingi za binafsi zimekuwa zikijihusisha na migogoro ya kung’ang’a nia madaraka wengine wakitaka ukuu wa shule na wengine ukurukenzi na hata wengine uhasibu, ” alisema Jaji Chacha.

Alimtaka Mulugo kuzitembelea shule binafsi za serikali mkoani Mbeya ili kubaini  zenye
migogoro na matatizo mengine ya kitaaluma na kuzifungia ili kuepusha madhara kwa wanafunzi.

Mulugo alisema kuwa atafanya ziara hiyo ya kushtukiza katika shule hizo bila kutaja ni lini  ili kubaini matatizo yaliyopo.

Katika harambee hiyo zaidi ya Sh. milioni 100 zikiwamo fedha taslimu na ahadi zilichangwa.

CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment