dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, June 15, 2013

SMZ: Kuna njama za kugombanisha waumini Zanzibar

NA MWINYI SADALLAH

15th June 2013


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi,Omar Yussuf Mzee
Matukio ya kupigwa risasi na kumwagiwa tindikali viongozi wa dini na serikali Zanzibar yalilenga kuleta fitina na kugombanisha waumini wa madhehebu ya dini Visiwani Zanzibar, imefahamika jana.
Tamko hilo limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi Omar Yussuf Mzee, Wakati akiwasirisha makadirio na matumizi ya bajeti ya serikali katika mwaka wa Fedha wa 2013/20 14.
Waziri Mzee, alisema vitendo vya hujuma dhidi ya viongozi wa dini na serikali vinakwenda kinyume na misingi ya haki za binadamu na kuwataka waumini na wananchi kuendelea kuwa na moyo wa subira na kulinda amani na Umoja wa kitaifa kwa manufaa ya Zanzibar.
Waziri Mzee alisema bila ya busara na hekima za viongozi wa dini na wananchi Zanzibar ingeweza kuingia katika machafuko makubwa na kuathiri kuathiri usitawi wa maendeleo ya wananchi wake.
Viongozi waliohujumiwa kwa kumwagiwa tindikali ni Katibu wa Mufti Sheikh Fadhili Soraga na sheha wa Tomondo Mohamed Kidevu,  wakati Padiri Ambrose Mkenda alipigwa risasi na mwezake Padri Evaristus Mushi, alipoteza maisha baada ya kupigwa risasi Febuari 17 mwaka huu wakati akienda kuongoza misa ya Jumapili huko Kibweni mjini Zanzibar.
“Mheshimiwa Spika serikali bado inaendelea na jitihada za kuwapeleka wahusika katika mikono ya sheria, tuendelee kunasihiana katika kudumisha utulivu tuliouonesha wakati wachache wetu walipotutia majaribuni,” Alisema Waziri Mzee.
Alisema mwenyezi Mungu atawalipa wote waliotenda uovu na dhuluma dhidi ya viongozi wa dini na kusisitiza nchi yoyote duniani haiwezi kufanikiwa kimaendeleo bila ya kuwepo kwa misingi ya amani na umoja wa kitaifa kwa wananchi wake.
Kuhusu mabadiliko ya katiba mpya alisema kwamna ni jambo la faraja kuona mchakato huo unaendelea kufanyika katika mazingira ya amani na utulivu kwa wananc hi wa Tanzania bara na Zanzibar.
Aidha alisema kwamba jambo la muhimu ni kuhakikisha mageuzi ya katiba mpya ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hayafarakanishi wananchi wake wa pande mbili za muungano huo.
Kuhusu bajeti, waziri Mzee aliserma SMZ  imepanga kutumia asilimia 37 ya bajeti kuu kufanikisha vipaumbele vine ikiwemo kuimarisha kiwango cha ubora wa elimu, afya, hasa upatikanaji wa dawa muhimu za binadamu, huduma za maji safi pamnoja na kufanikisha mpango kazi wa ajira kwa vijana ambapo  serikali imepanga kutumia shilingi Bilioni 113 .2 kufanikisha vipaumbele hivyo.
Tangu baadhi ya wanasiasa na wana harakati kuanza kampeni za kutaka Zanzibar kujitenga katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kumekuwepo na matukio mengi ya hujuma dhidi ya viongozi wa dini kupigwa risasi na kumwagiwa tindikali Visiwani Zanzibar.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment