zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, September 6, 2013

CUF kinaiunga mkono kambi ya upinzania Bungeni kukataa kujadili mswaada wa marekebisho

Written by   //  05/09/2013 
Chama cha wananchi CUF kimesema kinaiunga mkono kambi ya upinzania Bungeni kutokana na hatuwa walioichukua ya kukataa kujadili mswaada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba mpya ambao umesomwa kwenye Bunge hilo mjini Dodoma kwa ajili ya kujadiliwa na wabunge ndani ya bunge hilo hadi pale Zanzibar itakaposhirikishwa kikamilifu katika mchako huo.
Kauli hio imesemwa na mkurugenzi wa haki za Binadamu habari,uenezi na mawasiliano ya umma Mh:Salim Bimani wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake Vuga mjini Unguja.
Amesema kuwa jambo la kusikitisha kamati maalumu ya katiba na sheria ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ilifanya jitihada za kusikiliza maoni ya watu wengi sana pamoja na asasi mbali mbali za kiraia lakini wote nikutoka upande wa Tanzania Bara tu,kamati hio kwa makusudi ilifuta kabisa ratiba ya kuja kukushanya maoni kwa upande wa Zanzibar ili kuwasikiliza wazanzibar nao wanasemaje juu ya suala hili,
lakini kutokana na kutoitakia mema Zanzibar hawakufanya hivi wakati wanajua fika kuwa Zanzibar ni nchi moja iliounda jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Alieza kwa masikitiko makubwa wakati wabunge wa CUF wakitetea hoja hii ya kutaka mswaada huu uondolewe ndani ya Bunge ambao umewasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Mkoani,Mkoa wa kusini Pemba Mh,Ali Khamis Seif na kuungwa mkono kwa asilimia mia moja na chama cha CHADEMA,na NCCR Mageuzi,lakini cha ajabu na chakushangaza wabunge wa CCM kutoka Zanzibar wakiongozwa na Mbunge wa jimbo la Kitope Baloz Seif Ali Idi ambae ametoa barua kwa tume hio kwa niaba ya wazanzibar kuwa wamekubaliana na mswaada huo tena bila hata ya wazanzibar wenyewe kuulizwa juu ya suala hilo.
‘’Ni wazi kabisa hawa jamaa hawana nia njema na nchi hii na kuna kila haja ya kuwapinga kwa njia yoyote hile umeona wapi mtu asiekuwa na uchungu na nchi yake kama si dalali wa nchi unadhani ninani’’alieleza Bwana Bimani.
Pamoja na hayo ametowa wito kwa wananchama wa CUF wote pamoja na wazanzibar wanaoipenda nchi yao tena bila kubaguwana wawaunge mkono wabunge wao pamoja na wale wote wnanoshirikiana kuitetea Zanzibar.
Chanzo: Mzalendo

No comments :

Post a Comment