NA MWANDISHI WETU
9th September 2013
Akitoa rai hiyo wakati akizindua tawi la benki ya UBL jijini Dar es Salaam juzi, ambapo alisema taasisi za fedha zina wajibu wa kuwasaidia wananchi kwa kuwapatia mikopo bila masharti magumu.
Alisema serikali inatambua uwapo wa sekta za fedha na kwamba zina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.
Benki hiyo ambayo ipo jijini Dar es Salaam imefunguliwa kwa mara ya kwanza hapa nchini na kwa Bara la Afrika inapatikana Tanzania pekee.
Dk. Bilali aliitaka UBL kufungua matawi katika maeneo mengine hapa nchini ili kuwafikia wananchi wengi zaidi hususani waliopo vijijini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa UBL, Zamees Ghdrey alisema watahakikisha wanawafikia wananchi wengi ili kuwapatia huduma ya kifedha.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment