zanglassworks

AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, September 2, 2013

Polisi watumia mabomu kuwatawanya wananchi

NA IDDA MUSHI

2nd September 2013


Kamanda wa Polisi Mkoa, Faustine Shilogile
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Morogoro jana walilazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi, wakazi wa Kijiji cha Doma wilayani hapa baada ya kufunga barabara ya Iringa- Morogoro kwa mawe na magogo na kusababisha mamia ya abiria kukwama kwa saa saba.

Askari hao walichukua hatua hiyo kutokana na wakazi wa kijiji hicho kugoma kufungua barabara hiyo wakishinikiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, kwenda kusikiliza kero za wafugaji kugeuza mashamba yao malisho ya mifugo.

Abiria hao baada ya kukwama kwenye eneo hilo kuanzia saa 3 asubuhi, kufuatia barabara hiyo kufungwa askari hao walifika kwenye eneo hilo na kuwatawanya kwa mabomu baada ya kukaidi amri ya kuwataka waondoke. Baada ya polisi kuwatawanya kwa mabomu ya machozi, walitoa mawe na magogo na kuruhusu msururu mkubwa wa magari yakiwamo mabasi ya abiria kuendelea na safari.

Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Eliya Ntandu, aliyemwakilisha mkuu wa mkoa, akiambatana na Kamanda wa Polisi Mkoa, Faustine Shilogile, walifika eneo la tukio na kujaribu kuwatuliza wakazi hao waliokuwa wamebeba mawe na chupa bila ya mafanikio.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, walikubali kufungua barabara hiyo kwa masharti ya kutaka viongozi hao kwenda  kwenye mashamba yao kushuhudia uharibifu unaofanywa na wafugaji.

Hata hivyo, baada ya kwenda kwenye mashamba ya wananchi katika Kijiji cha Msongozi, viongozi hao hawakukuta mazao yaliyoliwa, isipokuwa mashamba yasiyo na mimea yalikuwa na kinyesi cha mifugo.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment