NA MWANDISHI WETU
23rd September 2013
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo la Kituo cha Jamii na Watoto katika eneo la Welezo Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja jana, Dk. Shein alisema imebainika kuwa maambukizi mapya ya Ukimwi kwa vijana yanahusishwa na matumzi ya dawa hizo.
“Katika miaka ya hivi karibuni imebainika kuwa maambukizi mapya ya Ukiwmi yanawakumba zaidi vijana wanaotumia dawa za kulevya hapa nchini, ” alisema Dk. Shein.
Kituo hicho kimejengwa na Jumuiya ya Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Zanzibar ZAPHA+ kwa msaada wa Taasisi ya Stephen Lewis Foundation ya Canada ambayo ilichangia Sh. milioni 43.65 ambazo ni sawa na asilimia 40.45
Shein alitoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali na washirika wengine katika mapambano dhidi ya Ukimwi na dawa hizo ili kuiokoa jamii hasa vijana ambao ni tegemeo la taifa.
Alisema tangu Ukimwi ulipogunduliwa, SMZ imekuwa ikifanya kila lililo ndani ya uwezo wake kuhakikisha Zanzibar haipati maambukizi mapya na kukomesha unyanyapaa dhidi ya wanaoishi na virusi hivyo.
Akizungumzia kuendelea kupungua kwa misaada ya wafadhili kwa shughuli za Ukimwi, Shein ameahidi kuwa Serikali itaendelea kutafuta namna bora ya kusaidiana na taasisi kama ZAPHA+ ili kutekeleza majukumu ya mapambano dhidi ya virusi hivyo.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment